Akithibitisha taarifa hizo, kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha, alisema, maafa hayo yametokea katika kijiji cha Mwakata, kata ya Isaka, wilayani Kahama na kwamba watu wengine 60 wamejeruhiwa vibaya huku mifugo kadhaa, ikiwemo Ng'ombe, Mbuzi na kuku, navyo vimekumbwa na maafa. Huenda idadi ya waliokufa ikaongezeka, kwani zoezi la uokoaji linaendelea licha ya changamoto ya kutokuwa na vifaa vya kutosha vya uokozi.
Wednesday, March 4, 2015
MVUA KUBWA ILIYOAMBATANA NA UPEPO MKALI YASABABISHA VIFO SHINYANGA
WATU 39 wamekufa, baada ya kuangukiwa na nyumba zao, kufuatia mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na upepo mkali kunyesha wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga, Jumanne usiku wa kuamkia leo Machi 4, 2015.
Akithibitisha taarifa hizo, kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha, alisema, maafa hayo yametokea katika kijiji cha Mwakata, kata ya Isaka, wilayani Kahama na kwamba watu wengine 60 wamejeruhiwa vibaya huku mifugo kadhaa, ikiwemo Ng'ombe, Mbuzi na kuku, navyo vimekumbwa na maafa. Huenda idadi ya waliokufa ikaongezeka, kwani zoezi la uokoaji linaendelea licha ya changamoto ya kutokuwa na vifaa vya kutosha vya uokozi.
Akithibitisha taarifa hizo, kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha, alisema, maafa hayo yametokea katika kijiji cha Mwakata, kata ya Isaka, wilayani Kahama na kwamba watu wengine 60 wamejeruhiwa vibaya huku mifugo kadhaa, ikiwemo Ng'ombe, Mbuzi na kuku, navyo vimekumbwa na maafa. Huenda idadi ya waliokufa ikaongezeka, kwani zoezi la uokoaji linaendelea licha ya changamoto ya kutokuwa na vifaa vya kutosha vya uokozi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
1 comment:
hizi ni mvua za awali tu, je Serikali na miundo mbinu mko wapi bado mvua halisi za masika hazijaingia!! shughulikeni pungezeni siasa uchwra!!
Post a Comment